"Mamkubwa unasema kweli?" Camira aliuliza kwa mshangao kidogo.
"Ndio kipenzi, jiandae utakuja kuchukuliwa kesho mapema, unaenda mjini na utakuwa huko ukifanya kazi vizuri, sawa kipenzi?" mama mkubwa alisema kwa sauti ya kuelekeza.
"Sawa mamkubwa, nakuahidi kuwa nitafanya vizuri, na nitawatumia hela na vitu vizuri kutoka Dar."
"Haya sasa ujue tunakutegemea wewe tuu. Si unaona maisha yetu yalivyo mwanangu? Ndugu zako wote wanakutegemea wewe, na usituangushe sawa?"
"Sawa mamkubwa, sitowaangusha. Hiyo ni ahadi yangu kwenu. Nitafanya chochote kuhakikisha siwaangushi. Ninakumbuka maisha yaliyopita, tulilipata pamoja tulikula pamoja, na janga kama njaa tulilala pamoja. Hata mama mzazi alifariki kwa kukosa matibabu kwa sababu hatukuwa na uwezo wa kumpeleka hospitali. Inaniuma sana mamkubwa leo hii mimi sina mama kutokana na kukosa pesa. Nimeamini kuwa kukosa pesa ni kitu kibaya sana, hivyo nitajituma sana."
"Nafurahi kusikia umejifunza hivyo, hautotuangusha. Sasa nenda ukalale, kesho mapema yule dada atakuja kukuchukua. Upange nguo zako kabla hujalala sawa?"
"Sawa mamkubwa."
Soma, sikiliza na tazama sehemu zote za hadithi, katuni na video kwenye tovuti ya Story Space.
Endelea Kwenye Tovuti© 2026 Story Space